Saturday, April 14, 2012

KONY 2012 - ONLY 5 DAYS LEFT FOR THE WORLD TO KNOW!

To see real time reports on LRA activity in the D.R.Congo, Central African Republic and South Sudan visit: http://www.lracrisistracker.com/

Website: www.kony2012.com
Youtube link: http://www.youtube.com/watch?v=Y4MnpzG5Sqc
Let the world know, Let us make a difference, let the responsible people take action and put an end to this!
RegardsFarry Thompson

BIBI CHEKA WA TMK WANAUME AKIFANYA VITU VYAKE HUSIKU HUU NDANI YA KILI MUSIC AWARDS


HAFLA YA TUZO ZA KILI MUSIC AWARDS 2012 NDANI YA MLIMANI CITY JIJINI DAR



Mshindi wa tuzo ya Wimbo Bora wa Zouk Rhumba,Ali Kibaa akikabidhiwa tuzo yake na Mwanadada Dina Marios wa Clouds Fm na Mkongwe Rainfred Masako wa ITV.
 Muwakilishi wa kundi la Arusha Gold akipokea tuzo ya Wimbo bora wa Ragga,kutoka kwa mwanadada Khadija Mwanamboka.
 Wasanii wa Muziki wa Ragga kutoka jijini Arusha wafahamikao kwa jina la Arusha Gold wakitoa shukrani kwa wadau wao waliowapigia kura mpaka kupata ushindi huo.

 Waendeshaji wa hafla hii usiku huu ni Milard Ayoo na mwanadada Vanessa Mdee.
 Burudani kutoka kwa vijawa T.H.T.
 Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar usiku huu ukiwa umefurika kwa washabiki wa muziki nchini ikiwa ni siku ya utoaji wa tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2012.
 Mchekeshaji wa Ze Komedi,Mpoki akitambulisha moja kikundi ya utumbuizaji usiku huu.
 Vijana wa T.H.T wakitoa burudani usiku huu.

Friday, April 13, 2012

 MSANII wa muziki bongo anayefanya kazi zake Nairobi Kenya, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amedai kuwa anatamani kurudi nyuma na kuendelea na kazi yake ya awali ya utangazaji na u-Dj kwa madai kuwa bado anauwezo mkubwa na kazi hizo.

Akiongea na mwandishi wetu kwa njia ya mtandao, Ray C, anaamini fani hiyo ya utangazaji bado anaiweza hivyo anafikiria kurejea bongo na kuendelea na kazi hiyo katika kituo atakachoamua kuomba kufanya kazi.

Ray C, awali kabla hajaanza muziki alikuwa akitangazaji pia Dj, katika kituo cha redio Clouds FM akiwa na kipindi chake cha miziki ya Hip Hop, R&B na Taarab ambapo alichokipa jina la “Dr Beat”.

“Kuna watu hawajui kama mimi niliwahi kufanya kazi hii, lakini kazi yangu ya kwanza kufanya ilikuwa ndiyo hii tena baada ya kumaliza elimu yangu ya Sekondari tu,” alisema.

Hata hivyo anadai kuwa anapenda kujifunza zaidi U-Dj, kwani fani hiyo anayeipenda kuliko kitu kingine chochote ingawa si zaidi ya muziki anaofanya.

Na Laurent Samatta
 KUNDI la muziki wa kizazi bongo, ‘Sold Graund Family’, linaloundwa na nyota kama Raphael Masaki ‘PDP’, Hamad Ramadhan ‘Hamaguy’, Big Black, Vicent Fransis ‘Master V’, limeachia ngoma ya mpya inayokwenda kwa jina ‘Happy Birthday’, ambayo kwa sasa imeanza kuchezwa redioni.

Kundi hilo lilipotea kwa muda ambapo wimbo huo ni ujio wao mpya, huku wakiwa katika mchakato wa kuachia albamu yao mpya ambayo bado hawajaipa jina hadi sasa.

Mmoja kati ya nyota wanaounda kundi hilo, Big Black, alisema kuwa albamu hiyo itakuwa na nyimbo nane ambazo ni ‘Happy Birthday’, ‘Masengenyo’, ‘Wajanja wa Bushi’, ‘Nyotera’, ‘Turuke Ngoma’ na nyingine kibao.

“Kila kitu kipo tayari na wimbo wetu unafanya vizuri sokoni hivyo tunaimani albamu yetu itakuwa na ngoma nyingine kali ambazo zitafanya vizuri,” alisema.

Hata hivyo aliongeza kuwa albamu yao inaweza kuwa sokoni mapema mwezi June kwani kwa sasa wanahitaji kumaliza mchakato wote wa kurekodi.

Na Laurent Samatta

 BABA mzazi wa msanii wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ,ameitaka jamii kutomhukumu mwanawe kutokana na kifo cha msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba, badala yake iache vyombo vya sheria vifanye kazi yake.

Mzazi huyo, Michael Edward Kimemeta anayeishi mjini Moshi, amewaomba Watanzania kuiachia Mahakama iamue kama mtoto wao anahusika katika kifo hicho ama la.

Kimemeta, ameeleza kuwa binti yake ana umri wa miaka 16 tofauti na inavyoelezwa kuwa ana miaka 18.

Juzi Lulu alifikishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka ya mauaji ya msanii mwenzake, Kanumba.

Kumekuwa na utata uliojitokeza kuhusu umri wa Lulu. Wakati mwenyewe akieleza kuwa ana miaka 17, Jeshi la Polisi lilieleza kuwa umri wake ni miaka 18 na juzi Mahakama iliambiwa kuwa msanii huyo ana umri wa miaka 17 na baba yake akisema ana miaka 16.

Kwa upande wake, mama mzazi wa Lulu Lucresia Karugila, alisema tukio la kifo cha Kanumba na kukamatwa kwa binti yake  Lulu, limempa mshituko mkubwa na kumsababishia maradhi ya kisaikolojia na kimwili.

“Hayo yaliyotokea kwa kweli yamenifanya niumwe kabisa hapa sasa hivi nimelala naumwa…nimempa go ahead (ruksa), baba yake azungumze kwa sababu taarifa zote anazo. Naomba mimi mniache kwa sasa,”alisema.

Kimemeta aliliambia Mwananchi jana kuwa mwanawe huyo alizaliwa Aprili 17 mwaka 1995 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

“Nataka nikuambie (mwandishi) mwanangu atatimiza umri wa miaka 17 ifikapo Aprili 17 mwaka huu. Sasa ana umri wa miaka 16 na ni mtoto. Tunavyosikia Kanumba alikuwa mpenzi wake inatuuma sana,” alisema.

Baba huyo alisema alizaa na mama yake Lulu lakini hawakuwahi kuishi pamoja. “Mwanamke huyo alikuwa akifanya kazi Shirika la Ndege Tanzania (ATC) na muda wote Lulu alikuwa akiishi na mama yake jijini Dar es Salaam,”alisema Kimemeta.

Ameomba familia ya marehemu Kanumba ikubali kupokea pole ya familia ya Lulu kupitia gazeti hili kutokana na mazingira kutoruhusu familia hizo kukutana.

“Nasikitika mazingira ya tukio lenyewe mpaka sasa hayaruhusu familia yetu kwenda kutoa pole na kuifariji familia ya Kanumba kulingana na utamaduni wa mwafrika…tunaomba wapokee pole zetu kupitia njia hii,” alisema.

Kwa mujibu wa Kimemeta, hivi sasa wanahofia maisha yao kutokana na jamii kujenga mtazamo hasi juu ya tukio hilo hata bila ya kusubiri vyombo vya sheria kusikiliza ushahidi wa tukio hilo na kutoa hukumu yake.

Alisema kuwa jamii inapaswa ifahamu kuwa, kikatiba mtu yeyote anayeshitakiwa kwa kosa lolote haimaanishi tayari ni mkosaji, bali atahesabiwa kuwa mtuhumiwa hadi pale Mahakama itakapomtia hatiani.

“Yanasemwa mengi mara ooh Kanumba ndio alianza kumpiga mwanangu mara ooh Kanumba alisukumwa …mimi nasema tuiache Mahakama hata sisi hatupendi mtu auawe, lakini Mahakama iachwe itende haki,”alisisitiza.

Akizungumzia maisha ya mwanawe Lulu, Kimemeta alisema alipokuwa akitangaza Kipindi cha Watoto Televisheni ya ITV, walifarijika sana, lakini alipoanza kuingia kwenye sanaa ya filamu, walijua sasa wamempoteza.


“Baada ya kuingia kwenye sanaa ya maigizo niliona kabisa tumempoteza mtoto na nilimweleza mama yake kuwa wale aliokuwa nao katika maigizo akiwamo Kanumba mwenyewe, nilikuwa siwaamini hata kidogo,”
 alisema.

Kimemeta alidai kuwa siku moja mwanawe alimpigia simu akimwarifu kuwa alikuwa anakwenda jijini Arusha kurekodi filamu na Kanumba, yeye alipinga safari hiyo akitaka Kanumba amthibitishie usalama wa binti yake.

“Kwa sababu nilikuwa sipendezwi na hayo mambo nilimwambia mama yake azungumze na Kanumba na akatuhakikishia atamlinda na kambi yake ina maadili, lakini kumbe huo ndio ukawa mwanzo wa mwanaye kugeuzwa mpenzi wa msanii huyo,”alidai.

Baba huyo mzazi alidai kutofanya vizuri darasani kwa mtoto wake huyo, kulichangiwa na hatua ya kuingia katika sanaa ya uigizaji.

“Lulu alikuwa mtoto mwenye tabia nzuri sana hata alipokuwa ITV kwa kweli alitutia moyo wazazi wake kwa jinsi ITV walivyokuwa wakimlea, lakini alipojiingiza tu kwenye uingizaji hapo ndipo mambo yalipoharibika,” alisema.

Alikanusha madai kuwa mwanawe hakumaliza kidato cha nne na kusisitiza kuwa Lulu alisoma Shule ya Kimataifa ya St Mary’s na baadaye alihamia Shule ya Sekondari ya Midway High School na kumaliza kidato cha nne mwaka jana.

Alisisitiza kuwa katika mambo yaliyokuwa yakiwaumiza mioyo, ni namna mtoto huyo alivyozidi kuharibika kwa kuingia katika fani ya uigizaji filamu.

Alisema angependa kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili azungumze naye kama rafiki yake na watafute suluhisho la maadili kwa kizazi cha sasa na cha baadaye.

Alisema tayari ameanza mchakato wa kuonana na Rais Kikwete ili amweleze siri aliyodai ni ‘nzito’ na kudai tayari ametafuta wazee watatu wenye busara wa kumsindikiza, endapo Rais atakubali ombi lake.

Pia ameziomba taasisi zinazojishughulisha na masuala ya haki za binadamu na msaada wa kisheria, kujitokeza na kumsaidia mwanawe.

Lulu alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam juzi na kusomewa shitaka la kumuua Kanumba, tukio lililotokea Aprili 7 mwaka huu eneo la Sinza Vatican.

Msanii huyo hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mauaji na hivyo alipelekwa rumande Gegeza la Segerea hadi Aprili 23 mwaka wakati kesi hiyo itakapotajwa.

Kifo cha msanii huyo kimetikisa nchi  kutokana na umaarufu wake, akiwa ameigiza filamu 40 zilikuwa zikirushwa katika vituo mbalimbali vya televisheni ndani na nje ya nchi.

Kanumba alipanga kujenga shule

Katika hatua nyingine, Fidelis Butahe na Pamela Chilongola wanaripoti kuwa mchaguaji maeneo ya kupigia picha za filamu za msanii Kanumba, Rahim Khatib alisema marehemu Kanumba alinunua eneo la ekari 15 huko Mpiji mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa shule yake ya sekondari.

Khatib alisema Kanumba alikuwa na mpango huo muda mrefu na kwamba lengo lake lilikuwa kuwasaidia wanafunzi wa eneo hilo ambao hutembea muda mrefu kutokana na shule kuwa mbali na eneo hilo.

“Kanumba alikuwa na mipango mizuri katika maisha yake, kuna eneo kubwa alilonunua Mpiji ili ajenge shule ya sekondari,” alisema Khatib.

Alifafanua kuwa hadi anafariki dunia, aliacha kiasi cha fedha zaidi ya Sh 40 milioni katika Kampuni yake ya Kanumba The Great.

“Marehemu ameacha fedha zaidi ya Sh 40 katika kampuni yake, magari matatu na hivi karibuni alinunua jingine aina ya Toyota Land Cruiser, ”alisema Khatib.

Katika hatua nyingine Khatib alisema kifo cha Kanumba ni pigo kwa watu waliokuwa wakifanya naye kazi akiwemo yeye mwenyewe kwa kuwa walikuwa wakimtegemea kwa kiwango kikubwa.

Sintah naye alonga

Kwa upande wake msanii maarufu wa filamu nchini, Christina Manongi maarufu kama Sintah ambaye alikuwa mmoja wa wasanii wa kwanza kufika nyumbani kwa marehemu Kanumba muda mfupi baada ya msanii huyo kuanguka, alisema kuwa siku tano kabla ya Kanumba kufariki, alikuwa na hasira tofauti na alivyomzoea.

Sintah ambaye alikuwa na msanii huyo katika Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Jumapili ya Aprili mosi pamoja na mwigizaji mwingine, Steve Nyerere alisema kuwa kila alichokuwa akimuuliza Kanumba, alimjibu kwa ukali.


“Ni tofauti na nilivyomzoea, siku ile ya Jumapili tulikaa pale Leaders Club mpaka usiku sana na kila jambo nililokuwa nikizungumza naye alinijibu kwa mkato na ukali kweli, ilinishangaza,” 
alisemaSintah

Alifafanua kuwa moja ya mambo waliyokuwa wakizungumza na Kanumba ni pamoja na yeye kutaka kuacha uigizaji, suala ambalo marehemu Kanumba hakuliunga mkono na kumjibu kwa ukali kuwa asijitoe katika uigizaji.

Source: Mwananchi
JACO- R.I.P KANUMBA THE GREATE

NEW TRACK: GRACE MATATA FT WYRE -- UTANIFAA

We are aware of the fact that the fans of Grace have been waiting for far too long to hear her voice again. Well, the wait is over! Grace somehow managed to get Wyre —with more than a decade in the game — all the way from Kenya on this sensational song, below are the details:


Written by: Grace Matata & Wyre
Composed by: Grace Matata & Mujwahuki Kanye
Guitar by: Grace Matata
Produced, recorded and mixed by: Mujwahuki Kanye
 for M lab 2012

 


Thursday, April 12, 2012

STEVEN KANUMBA & MZEE KIPARAWALIPENDANA KAMA BABA NA MWANA…!!!  




 Enzi za uhai wao! Hapa ni wakati Kanumba alipo mtembelea mzee Kipara kigamboni wakati alipoanza kusumbuliwa na matatizo ya miguu mwaka jana. Dah kweli kifo hakichagui mpumzike kwa amani R.I.P Enzi za uhai wao wakipiga stori mbali mbali za hapa na pale.



Wednesday, April 11, 2012

TAMADUNI MUSIC UZINDUZI WA KANDAMSETO

KUWA WA KWANZA KUJIPATIA NAKALA YAKO YA MZIMU WA SHAABAN ROBERT, KANDAMSETO KUTOKA KWA NASH EMCEE, SIKU YA TAREHE 21/04/2012 PALE BAMAGA/KIJITONYAMA NDANI YA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KIINGILIO NI BURE ILA CD ITAPATIKANA KWA SHILINGI ZA TANZANIA ELFU SITA (6000/=)

Deepest Sympathies to the loss of "Steven Kanumba" + Banx Ft Gnako - Right Now

 Kwa kuanza ,Nitangulize our deepest Sympathies toka Noizmekah Production studios Arusha,May the Soul of the great Film icon "Steven Kanumba" rest in eternal peace,We all head the same path...Banxtramatic aka Hookmaster toka pande za ChugaTown na mtu mzima te kankara aka Gnako wanakuja na banger waloipa jina "Right Now" ikiwa ni 1st solo project ya banx kuwa officially released kwa hewa,Kama inavofahamika wara na banx waliskika pamoja kiping\di cha nyuma kidogo katika pini la Right here alokuwemo pia mzee mzima Umbwa 4rom Watengwa "Nimekuwa quiet kw muda na hii ni tokana na majukumu ya kielimu zaidi na this joint ni exclusive kwa watu wangu wote round the world,mkono ni wa Defxtro pande za noizmekah.com,Peace kwa supporting media zote ndani na nje ya BongoTz!!..once again,Rest In peace to all our lost loved ones!

NEW TRACK: Moplus & JCB ft Banx - Everywhere we go

 Moplus na JCB wamshirikisha Banx katika brand new collabo iloundwa pande za noizmekah.com,mdundo ukiwa wa producer Mosco na vocal mixing Defxtro,Everywhere we go ni motivational hiphop joint fo all ya'll hiphop fans out there,kwa mujibu wa taarifa zilizowahi kutolewa na MC's hawa ni kuwa hii collabo ni moja kati ya zingine saba ambazo kwa pamoja zitakuwa katika compilation mixtape ya pamoja!!

NEW TRACK: BouNako FiDo MoPlus Frost GeeZ LavosT & RitchiE - Gangsta

Pini hili la  "Gangsta",ni collabo kati ya hiphop Mc's anzia Dar-Arusha-Mombasa mpaka Nairobi.Artists walopita ni BouNako, FiDo, MoPlus, Frost ,GeeZMabov, LavosT na RitchieRich,Hiphop ni worldwide na tunafanya kazi kwa pamoja kuimarisha game na mshikamano ambao upo kati yetu wasanii,Geez Mabov anarepresent Dirty South pande za DSM,FiDo,MoPlus,Frost na BouNako wanarepresent Arachuga,Lavosti toka Ukoo MauMau anarepresent Mombasa na RitchieRich toka HeadBangaz International akirepresent pale Nairobi City,Audio ikiwa imesmamiwa pande za Noizmekah Studios,Video ya pini hili inaendelezwa editing Pande za RED Films Arusha..

LULU MICHAEL BAADA YAKUFIKISHWA MAHAKAMANI.

 Habari hii na BBC Swahili

Msanii wa kike wa filamu Tanzania Elizabeth Michael Kimemeta maarufu kama Lulu,amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya msanii mwingine wa filamu Marehemu Steven Kanumba.
Amefikishwa mahakamani ikiwa ni siku nne, tangu alipokamatwa mara baada ya kifo cha msanii huyo ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.
Mbele ya Hakimu mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam,Bi Augustina Mbando,Elizabeth Michael Kimemeta ajulikanaye kama Lulu kwa jina la Usanii,aliwasili mahakamani hapo akiwa chini ya Ulinzi mkali wa askari Polisi waliokuwa wamevaa kiraia na wengine wakiwa wamejihami kwa silaha.
Mara baada ya Kufikishwa mahakamani,upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa serikali Bi Elizabeth Kaganda ulimsomea shtaka moja ambalo ni la mauaji, kosa ambalo ni kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu kifungu cha 196.
Wakili huyo wa serikali Bi Elizabeth Kaganda,alidai mbele ya mahakama kuwa mnamo tarehe 07 mwezi April mwaka 2012,katika eneo la Sinza Vatican,msanii Elizabeth alimuua msanii Steven Kanumba.
Akiwa amevalia gauni kubwa lijulikanalo kama dera lenye rangi ya Njano mtandio wa rangi ya waridi na kandambili nyekundu mshtakiwa alionekana kutokuwa na wasi wasi pamoja uzito wa tuhuma za mauaji anayokabiliwa nayo huku akijibu maswali kadhaa kuhusu wasifu wake.
Msanii huyo alikanusha kuwa na umri wa miaka 18 baada
kuulizwa ,ambapo yeye amesisitiza kuwa ana umri wa miaka 17, hii ikiwa ni tofauti na habari ambazo zimekuwa zikiripotiwa kuhusu umri wa msanii huyo ambaye sasa anatambulika kama mshtakiwa.
Kesi hii ya mauaji inatajwa kwa mara ya kwanza na mshtakiwa hakutakiwa kukiri wala kukana mashtaka.
Upande wa mashtaka umeieleza mahakama kuwa kesi bado iko kwenye upelelezi ambapo inatarajiwa kutajwa tena April 23 mwaka huu.
Mshtakiwa amepelekwa rumande hadi siku hiyo wakati kesi hii itakapotajwa tena.
Kwa upande mwingine tukio la kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo kumefanywa kwa usiri mkubwa na kufanya waandishi wa habari wengi wameshindwa kufuatilia kwa karibu tukio lenyewe.
Kufikishwa mahakamani kwa msanii huyo na kusomewa shtaka la mauaji ya Kanumba kumetokea siku moja baada na Marehemu Steven Kanumba kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni.
Mazishi yake yalichukua sura ya kitaifa kutokana na umaarufu aliojijengea msani huyo katika jamii ya watanzania na hata nchi za nje.

DEDICATION AND TRIBUTE TO STEVEN KANUMBA)

 

TISHIO la TSUNAMI linaweza kutokea pwani ya Tanzania kuanzia saa 1 leo usiku,


 Pichani ni maeneo ya Makumbusho yalivyo kwa sasa hivi


kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha sasa hivi hapa Dar es Salaam mamlaka ya hali ya hewa imesema tishio la Tsunami linaweza kutokea pwani ya Tanzania kuanzia saa 1 usiku na saa 3 usiku leo. 
Sehemu nyingine zitakazo weza pata Tsunami ni SEYCHELLES, PAKISTAN, SOMALIA, OMAN, MADAGASCAR, IRAN, UAE, YEMEN, COMORES, BANGLADESH, MOZAMBIQUE.

TUMEJIFUNZA NINI KATIKA MSIBA WA KANUMBA SISI VIJANA?

 Kanumba kazikwa hivyo kwa sababu nyingi sana baadhi ni kwamba

1.Ni mmoja ya msanii ambaye hakuwa na skendo ambazo zilikuwa zinaleta picha mbaya katika jamii na katika Tasnia hiyo ya Filamu na hata pale waaandishi walipotaka kuuza Gazeti aliwakemea huyo ni msanii makini sana
2.Hakuwa mbinafsi kwani tumeshuhudia vijana wengi kawaibua katika Filamu zake mbalimbali
3.Hakuwa na Majivuno Kwa kiwango alichokuwa amefika Kanumba leo angetafuta watu fulani wa kuongea nao lakini hakuwa hivyo
4.Alipenda jamii ndiyo maana aliweza kutoa misaada mbalimbali kwa makundi tofauti na ndiyo maana Jamii imejitokeza katika kumuaga
5.Hakukatishwa na Maneno ya watu wasiopenda mafanikio ya wenzao
6.Aliipenda sana nchi yake kwa dhati na popote alipenda kusema natoka Tanzania
7.Kanumba hakubagua huyu wala yule ndiyo maana kazikwa na watu wengi wa rika tofauti
8.Alikuwa kiongozi kwa wenzake.
9.Alichukia umaskini.
0.Kanumba alijipenda na alipenda kutengeneza Historia hapa Duniani

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo niliyajua kwa Kanumba baada ya kuwa na Mafanikio ya haraka katika tasnia ya Filamu,nilitamani sana kufika katika mazishi lakini sikuweza,aaaaah Kanumba ipo siku nitafika kwenye kaburi lako japo niseme neno ambalo siku zote nilipenda nikwambie lakini sikuweza kukutana nawe na hilo neno ni hili hapa HONGERA KAKA KWA KAZI ZAKO hili neno sijakwambia lakini ipo siku nitakwambia tutakapokutana katika uzima wa Milele

 

 

 Mbunge wa kawe/Chadema Halima mdee yeye pamoja Mbunge wa viti maalum Ester Bulaya (CCM) jana walienda kumuona Lulu, na kwa wakati huu Mh Halima Mdee kupitia mtandao wa Tweeter anaendesha kampeni ya Kuchangisha Pesa za malazi kwa ajili ya familia ya Lulu (mama yake).
Mh.Halima mdee amesema kwamba lulu anahitaji mwanasheria makini wa kuweza kumnasua kwenye kesi hiyo, lakini pia anahitaji mwana saikolojia (psychological support) wa kuzungumza nae ili aweze kuwa fresh kiakili.


kwa wakati huu Lulu anashikiliwa katika kituo cha polisi Oysterbay


SOMA TWEETS ZA @HALIMA MDEE

Halima J Mdee ‏ @halimamdee


Watz wenzangu. Leo mimi na mhe. Bulaya tulikwenda kumuona Lulu oysterbay polisi. She really needs our support. Kwanza she is only 17..

Halima J Mdee ‏ @halimamdee


Pili anahitaji sana psychological support. Nawaomba watu wenye taaluma hiyo wasisite kwenda kumuona. wasiliana na 0714282527steve nyerere.

Halima J Mdee ‏ @halimamdee

Tatu anahitaji wanasheria makini wa kumsaidia. Kwa yeyote ambaye yuko tayari naomba awasiliane nami 0759569823..

Halima J Mdee ‏ @halimamdee

Nne,at that tender age ndio alikuwa anategemewa na familia yake. Now yuko ndani matatizo yamezidi kuwa makubwa.

Halima J Mdee ‏ @halimamdee

Kwa yeyote anayeguswa,naomba atume chochote kwenye namba hii 0754878890 ni namba ya m pesa ya mama yake Tumsaidie huyu mtoto!

Again ..Namba ya M -PESA kwa wanaotaka msaidia Binti yetu Lulu+255754878890.Ni namba ya mama yake!

Muigizaji wa Filamu nchini anaehusishwa na kifo cha Muigizaji Mwenzie,Marehemu Steven Kanumba,Bi Elizabeth Michael a.k.a Lulu amepandishwa kizimbani mapema leo asubuhi kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kwa kusomewa mashtaka yake kuhusiana na kuhusika kwa kifo cha Muigizaji huyo nguli hapa nchini.Elizabeth Michael amesomewa mashtaka hayo mbele ya hakimu Agustino Mmbando na wakili Elizabeth Kaganda ya mauaji ya Muigizaji wa Filamu nchini,Marehemu Steven Kanumba yaliyotokea huko sinza vatcan jijini Dar es Salaam april 7 mwaka huu.Elizabeth Hakutakiwa kujibu chochote Mahakamani hapo kwani mahakama hii haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.Kesi hiyo imeahirishwa na kupangwa kusikilizwa tena april 23 mwaka huu.Muigizaji huyo aliletwa mahakamani hapo kwa mwendo wa kasi kama mshale na kwa ulinzi mkali na pia ndivyo alivyoondolewa Mahakamani hapo kiasi kwamba hakuna hata mwandishi alieweza kupata picha ya Muigizaji huyo mwenye tuhuma za mauaji Na kupandishwa katika gari ndogo nyeupe aina ya suzuki grand vitara yenye nambari za usajiri T 848 BNV huku kwenye kioo nambari zake zikisomeka PT 2565.
UPATIKANAJIA WA MAJI MJINI KISARAWE BADO NI TATIZO

Upatikanaji huduma ya maji Kisarawe bado ni tatizo

Baadhi ya wakazi wa eneo la Kisarawe Mjini wakiwa wamepanga foleni ndefu za vyombo vya kutekea maji kwenye moja ya mabomba ya umma eneo hilo hivi karibuni. Kumekuwa na shida kubwa ya upatikanaji wa huduma za maji kwa matumizi ya nyumbani na shughuli nyingine za wananchi eneo la Kisarawe hasa Kata ya Maneromango iliyopo nje kidogo ya mji huo.
Na Joachim Mushi, Kisarawe
MGOGORO wa ukosefu wa maji ya matumizi ya nyumbani na shughuli nyingine bado ni kero kubwa kwa wakazi wa Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani hasa katika Kata ya Maneromango iliyopo nje ya Mji wa Kisarawe.
Uchunguzi uliofanywa na Mwanahabari Wetu hivi karibuni maeneo ya Kata ya Maneromango imebaini bado kuna shida kubwa ya maji kwa wakazi wa eneo hilo licha ya uwepo wa baadhi ya visima vya umma na watu binafsi vilivyochimbwa hivi karibuni.
Shida ya maji imepungua katika baadhi ya shule za msingi na sekondari pamoja na vituo vya afya pekee baada ya kujitokeza wafadhili kujenga mifumo ya uvunaji wa maji ya mvua katika shule hizo na kituo cha afya.
Shule ambazo awali zilikuwa na shida kubwa ya maji na sasa zimenufaika na msaada wa kujengewa mfumo wa uvunaji maji ya mvua eneo la Maneromango ni pamoja na shule za msingi, Mengwa na Maneromango, Shule ya Sekondari Maneromango pamoja na kituo cha Afya cha Maneromango.
Akizungumza na mtandao huu Said Mzara mkazi wa Kijiji cha Boga amesema unafuu wa kupatikana kwa maji hutokea mvua zinaponyesha tu ambapo wananchi wengi hupata maji lakini baada ya kipindi hicho shida ya maji hurejea kama kawaida.
“Wanaonufaika kwa kiasi kikubwa na huduma za maji ni shule za msingi na sekondari pamoja na kituo chetu cha afya ambao wamejengewa mfumo wa kuvuna maji ya mvua, ukweli ni kwamba bado wananchi tunaitaji msaada wa kuboreshewa huduma za maji hasa visima vya umma,” alisema Mzara.
Muhamed Omar mkazi wa Kitongoji cha Msegamo anasema ushauri wa kuvuna maji ya mvua unaotolewa na wataalam na baadhi ya viongozi ni mgumu kwa wananchi wengi kutokana na kumiliki nyumba za nyasi ambazo ni hafifu kwa uvunaji maji ya mvua.
“Wanashauri tuvune maji ya mvua suala hili ni gumu kwa asilimia kubwa ya wakazi kwani bado tunamiliki nyumba za nyasi, isipokuwa kwa wakazi wa mjini sasa kwa hali hii utavunaje maji ya mvua?,” alihoji Omar ambaye ni mkulima na mfanyabiashara ndogo ndogo.
Mwandishi wa habari hizi ametembelea pia maeneo ya katikati ya Mji wa Wilaya ya Kisarawe ambapo amebaini bado kuna shida kubwa ya maji kutokana na kubaini foleni kubwa za maji katika maeneo ya mabomba ya maji.
AFRICAMAGIC SWAHILI PAYS TRIBUTE TO STEVEN KANUMBA

AfricaMagic Swahili pays tribute to Steven Kanumba

AfricaMagic Swahili has announced that it will play tribute to popular Tanzanian actor Steven Kanumba whose tragic demise this past weekend has shocked and saddened movie fans across East Africa. 
As part of the memorial tribute the channel will screen a festival of his movies, beginning this weekend, as it honors his contribution to the African film landscape. Starting on Saturday April 14 at 19:30 EAT, viewers can tune in for UNCLE JJ, followed on Sunday April 15 at 20:00 EAT by THIS IS IT (part 1 and 2). 
Then on Saturday April 21 at 19:30 EAT audiences can see him in MORE THAN PAIN which will be followed on Sunday April 22 by YOUNG BILLIONAIRE (part 1 and 2). Rounding off the festival dedicated to the star will be the movie BLACK SUNDAY, to be screened on Saturday April 28 at 21:20 EAT.
 Applauding Kanumba for his talent, energy and determination M-Net Africa Managing Director Biola Alabi said, “We must celebrate this dynamic young man who lit up our screens and won the hearts of many. 
His passing is a loss to the African entertainment industry and we would like to extend our sincere condolences to his family, friends and loved ones.”

Tour Ya Mr. Blu MALAYSIA

NYOTA NDOGO AFIWA NA BABA YAKE MZAZI.

 Msanii wa muziki kutoka Mombasa Kenya Nyota Ndogo ampoteza babake leo asubuhi kule Muweza Tanga Tanzania na anatarajiwa kuzikwa kesho. Pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Mzee Abdallah.

Tuesday, April 10, 2012

PATA UKWERI JUU YA KIFO CHA STEVEN KANUMBA.KILICHOMUUA KANUMBA NI MTIKISIKO WA UBONGO (BRAIN CONCUSSION)-MADAKTARI WAELEZA

 Steven Kanumba.

Florence Majani na Suzzy Butondo wa Gazeti la Mwananchi

MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.

Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi…

Florence Majani na Suzzy Butondo wa Gazeti la Mwananchi
MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.
Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.
“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion,” alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) “Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka” alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.
“Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.”
“Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.”
Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo...

UZURI WA JENAZA LA MAREHEMU STEVEN KANUMBA 

 

Mama Kanumba aongea kuhusu marehemu mwanae na Nicolous Ngaiza

Tuesday, April 10, 2012

Mwili wa Marehemu Steven Kanumba ukipelekwa kaburini tayari kwa maziko

LIVE KUTOKA KINONDONI MAKABURINI KWENYE MAZISHI YA STEVEN KANUMBA

 Hii ni barabara ya Kinondoni kuingia kwenye makaburi ya Kinondoni ilikuwa ni balaaaa yani dah, kule mbele ndio mwili wa marehemu Steven Kanumba ndio unakuja

Kwa wingi wa watu ilibidi watu wapande juu ya miti lakini baadae waliamuriwa washuke chini na kamanda Kova



 Ray akiwa aamini kama swaiba wake ndio anakwenda kwenye nyumba yake ya milele



 Charlz Baba akiwa na wenzake kutoka Mashujaa Band, Charz ameniambia walikuwa wanatokea Morogoro so waliweza kuwahi makaburini